IMEWEKWA AGOSTI 10, 2013 SAA 3:01 USIKU
USHINDI wa mabao 3-1 ambao Arsenal imeupata leo kwenye Uwanja wa Olimpiki mjini Helsinki dhidi ya Manchester City katika mchezo wa kirafiki unamaanisha The Gunners wanaweza kuendelea na maisha bila Luis Suarez.
Arsene Wenger anahaha kusaka saini ya mshambuliaji huyo asiyefurahia maisha Liverpool akiwa ana matumaini makubwa ya kumpata Suarez, licha ya ofa yake ya Pauni Milioni 40 kupigwa chini.
Katika mchezo wa leo, mabao ya Arsenal yamefungwa na Theo Walcott dakika ya tisa, Aaron Ramsey dakika ya 59 na Olivier Giroud dakika ya 62, wakati bao la City limefungwa na Negredo dakika ya 80.
Kikosi cha Arsenal kilikuwa: Szczesny/Fabianski dk46, Sagna/Jenkinson dk73, Mertesacker, Koscielny, Gibbs, Arteta/Perez dk68, Ramsey/Hayden dk88, Wilshere/Cazorla dk46, Podolski/Giroud dk46, Oxlade-Chamberlain/Zelalem dk74 na Walcott
Manchester City: Hart, Zabaleta (Richards 46), Kompany, Lescott/Boyata dk86, Clichy, Milner/Navas dk46, Fernandinho/Rodwell dk80, Toure/Garcia dk68, Silva, Negredo/Jovetic dk68 na Dzeko/Nasri dk46.
Wakali wa Gunners: Theo Walcott na Aaron Ramsey waliifungia Arsenal leo
Mashabiki wa Arsenal
Yaya Toure akipambana na Aaron Ramsey
David Silva (kulia) na Mikel Arteta wakigombea mpira
Theo Walcott akimtungua Joe Hart kuifungia Arsenal bao la kwanza
Pablo Zabaleta na Alex Oxlade-Chamberlain (kulia) wakipambana
Vincent Kompany akijiandaa kuanzisha mashambulizi
Tayari? Mashabiki wa Arsenal wakitamba na bendera ya Finland mjini Helsinki kabla ya mechi
Carl Jenkinson akipambana na Samir Nasri
Kilaini namna hiyo: Aaron Ramsey akimtungua kipa Joe Hart
Amepagawa: Kiungo wa City, David Silva aliudhiwa na uamuzi wa refa kipindi cha kwanza
Walcott ameifungia Arsenal leo


.png)