KIUNGO Mnigeria, David Udoh jana aliichezea Simba SC katika mchezo wa Kundi B Kombe la Mapinduzi ikitoa sare ya bila kufungana na wenyeji, Mlandege SC Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Udoh kwa pamoja na winga Muivory Coast, Cheick Ahmed Tenena Moukoro na kiungo mwingine, Msudan Sharaf Eldin Shiboub wapo Simba kwa majaribio kupitia michuano hii ya Mapinduzi na atakayemvutia kocha Mspaniola, Pablo Franco Martin atasajiliwa.
0 comments:
Post a Comment