Nyota wa Borussia Dortmund, Jadon Sancho alionyeshwa kadi ya njano kwa kuvua jezi kuonyesha fulana yenye maandishi 'Justice for George Floyd' akilaani tukio la kuuawa kwa Mmarekani mweusi, George Floyd aliyeuliwa kikatili na Polisi. Sancho alifanya hivyo katika mchezo wa Bundesliga dhidi ya wenyeji, Paderborn jana Uwanja wa Benteler-Arena akifunga mabao matatu dakika za 57, 74 na 90 na ushei katika ushindi wa 6-1. Mabao mengine ya Borussia Dortmund yalifungwa na Thorgan Hazard dakika ya 54, Achraf Hakimi dakika ya 85 na Marcel Schmelzer dakika ya 89 wakati bao pekee la Paderborn lilifungwa na Uwe Hunemeier kwa penalti dakika ya 72 PICHA ZAIDI GONGA HAPA
Worried about your phone overheating? Here are some prevention tips
-
Hot phone? There are hacks for that.
1 minute ago



.png)
0 comments:
Post a Comment