• HABARI MPYA

    Friday, June 26, 2020

    LAMINE MORO AFUNGIWA MECHI TATU NA FAINI SH 500,000 KWA KUMPIGA TEKE MWINYI KAZIMOTO

    Na Mwandshi Wetu, DAR E SAALAM
    BEKI wa Yanga SC, Lamine Moro amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya Sh. 500,000 kwa kosa la kumkanyaga mchezaji wa JKT Tanzania, Mwinyi Kazimoto ambaye naye amefungiwa mechi mbili kwa kosa la kusababisha vurugu kwenye mchezo wao uliopigwa Juni 17, 2020 kwenye Uwanja wa Jamhuri Dodoma.
    Taarifa iliyotolewa na Bodi ya Ligi jana, imesema kwamba, Kamati ya Saa 72 pia imepokea malalamiko ya Azam FC kuhusu uamuzi uliofanywa katika mchezo wao dhidi ya Yangasc  na kuyapeleka kwenye Kamati ya Waamuzi.



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LAMINE MORO AFUNGIWA MECHI TATU NA FAINI SH 500,000 KWA KUMPIGA TEKE MWINYI KAZIMOTO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top