• HABARI MPYA

    Sunday, June 14, 2020

    AZAM FC WAIPIGA MBAO FC 2-0 NA KUJIWEKA SAWA NAFASI YA PILI KWENYE MSIMAMO WA LIGI KUU BARA

    Wachezaji wa Azam FC wakimpongeza mwenzao, Shaaban Iddi Chilunda baada ya kufunga bao la pili dakika ya 90 na ushei katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara wakiilaza Mbao FC ya Mwanza 2-0 usiku wa leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini Dar es Salaam, bao la kwanza likifungwa na Muivory Coast, Richard D'jodi dakika ya 49.
    Kwa ushindi huo, Azam FC inafikisha pointi 57 baada ya kucheza mechi 29, ingawa inabaki nafasi ya pili nyuma ya mabingwa watetezi, Simba SC wenye pointi 72 za mechi 29 pia, wakati vigogo, Yanga SC ni wa tatu kwa pointi zao 54 za mechi 28 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC WAIPIGA MBAO FC 2-0 NA KUJIWEKA SAWA NAFASI YA PILI KWENYE MSIMAMO WA LIGI KUU BARA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top