• HABARI MPYA

    Tuesday, February 20, 2018

    EL HILAL VITANI LIGI YA MABINGWA AFRIKA LEO IKITOKA KULALA 1-0

    TIMU ya El Hilal ya Sudan leo itakuwa nyumbani kuwakaribisha LISCR ya Liberia katika mchezo wa marudiano Raundi ya Awali Ligi ya Mabingwa Afrika.
    Hilal, moja ya timu zenye historia katika michuani ya klabu barani Afrika, itaingia kwenye mchezo wa leo ikikabiliwa na shughuli ya kupindua matokeo, baada ya kufungwa 1-0 kwenye mchezo wa kwanza Liberia.
    Jumla ya mechi tatu za marudiano Raundi ya Awali Ligi ya Mabingwa wa Afrika zinachezwa leo, nyingine ni kati ya wenyeji, Williamsville AC ya Ivory Coast na Stade Malien ya Mali ambazo mechi ya kwanza zilifungana 1-1 na Olympic de Bangui ya Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) itawakaribisha ES Setif ya Algeria walioshinda 6-0 kwenye mechi ya kwanza.
    El Hilal ya Sudan itakuwa nyumbani  leo kuwakaribisha LISCR ya Liberia

    Mechi zaidi za marudiano zitachezwa kesho, zikiwemo kati ya Saint Louis ya Shelisheli na Yanga SC ya Tanzania na El Merreikh ya Sudan na Township Rollers ya Botswana, ambazo washindi wake wa jumla watakutana katika hatua ifuatayo.
    Yanga ilishinda 1-0 kwenye mechi ya kwanza, wakati Township Rollers ilishinda 3-0 nyumbani pia.
    Saint Louis watakuwa wenyeji wa Yanga SC ya Tanzania nchini ya Shelisheli kesho

    MARUDIANO MCHUJO LIGI YA MABINGWA AFRIKA
    Jumanne Februari 20, 2018
    El Hilal (Sudan) vs LISCR (Liberia) (0-1)
    Williamsville AC (Ivory Coast) vs Stade Malien (Mali) (1-1)
    Olympic de Bangui (CAR) vs ES Setif (Algeria) (0-6)
    Jumatano Februari 21, 2018
    KCCA (Uganda) vs CNaPs Sport (Madagascar) (1-2)
    Mbabane Swallows (Swaziland) vs Bantu (Lesotho) (4-2)
    Aduana (Ghana) vs El Tahadi (Libya) (0-1)
    Mounana (Gabon) vs RC Kadiogo (Burkina Faso) (0-1)
    MFM (Nigeria) vs AS Real (Mali) (1-1)
    MC Alger (Algeria) vs AS Otoho (Kongo) (0-2)
    Horoya (Guinea) vs AS FAN (Niger) (3-1)
    Makkassa (Misri) vs Generation Foot (Senegal) (0-2)
    Saint Louis (Shelisheli) vs Yanga SC (Tanzania) (0-1)
    El Merreikh (Sudan) vs Township Rollers (Botswana) (0-3)
    Leones Vegatarianos (Equatorial Guinea) vs Gor Mahia (Kenya) (0-2)
    Esperance (Tunisia) vs Concorde (Mauritania) (1-1)
    Eding Sport (Cameroon) vs Plateau United (Nigeria) (0-3)
    AS Port (Togo) vs AC Leopards (Kongo) (1-2)
    Zesco (Zambia) vs JKU (Zanzibar) (0-0)
    ASEC Mimosas (Ivory Coast) vs Buffles (Benin) (1-1)
    UD Songo (Msumbiji) vs Ngaya (Comoro) (1-1)
    Be Forward (Malawi) vs AS Vita (DRC) (0-4)
    FC Platinum (Zimbabwe) vs Primeiro de Agosto (Angola) (0-3)
    Pamplemousses (Mauritius) vs Bidvest (Afrika Kusini) (0-2)
    Difaa El Jadida (Morocco) 10-0 Benfica (Guinea Bissau)
    Benfica (Guinea Bissau) vs Difaa El Jadida (Morocco) (0-10)
    Lydia Academic (Burundi) vs Rayon Sports (Rwanda) (1-1)
    Saturday, 24 February 2018
    Armed Forces (Gambia) vs Zanaco (Zambia) (0-3)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: EL HILAL VITANI LIGI YA MABINGWA AFRIKA LEO IKITOKA KULALA 1-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top