• HABARI MPYA

    Saturday, October 10, 2015

    MAZOEZI YA TAIFA STARS MCHANA WA LEO UWANJA WA KAMUZU

    Beki wa Tanzania, Taifa Stars, Hassan Isihaka akiwa hewani kupiga mpira kichwa katika mazoezi ya timu hiyo mchana wa leo, Uwanja wa nyasi bandia wa Kamuzu mjini Blantyre wakati wa maandalizi ya mwisho kabla ya mchezo wa marudiano dhidi ya wenyeji kesho kwenye Uwanja huo huo, hatua ya awali kuwania kupangwa kwenye makundi ya kuwania tiketi ya Kombe la Dunia mwaka 2018 nchini Urusi  

    Kiungo Said Ndemla akimiliki mpira mbele ya mshambuliaji Thomas Ulimwengu

    Viungo Himid Mao (kushoto) na Said Ndemla wakigombea mpira

    Mabeki Kevin Yondan (kulia) na Mohammed Hussein 'Tshabalala' wakiwania mpira wa juu

    Winga Farid Mussa akiambaa na mpira mbele ya Hassan Isihaka na Mbwana Samatta

    Kiungo Mrisho Khalfan Ngassa akinywa maji wakati wa mapumziko ya mazoezi hayo

    Kocha Charles Boniface Mkwasa akimuelekeza jambo Msaidizi wake, Hemed Morocco (kulia)

    Nahodha Nadir Haroub 'Cannavaro' (kushoto) akiwaongoza wenzake katika mazoezi ya kukimbia

    Baadhi ya viongozi na Watanzania waliokuja kuisapoti Taifa Stars mjini hapa

    Baadhi ya Watanzania waliokuja kuisapoti Taifa Stars mjini hapa
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAZOEZI YA TAIFA STARS MCHANA WA LEO UWANJA WA KAMUZU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top