• HABARI MPYA

    Sunday, April 05, 2015

    RONALDO APIGA TANO REAL MADRID IKIIFUMUA GRANADA 9-1 LA LIGA

    REAL Madrid imefanya kufuru La Liga, baada ya kuifunga mabao 9-1 Granada mchana wa leo, huku Mwanasoka Bora wa Dunia, Cristiano Ronaldo peke yake akifunga mabao matano.
    Ronaldo alitumia dakika nane kufunga hat-trick kipindi cha kwanza katika dakika za 31 36 na 38 na sasa amemfikia Lionel Messi wa Barcelona kwa kufunga hat-tricks  24 kila mmoja La LigaNyota huyo wa Ureno aliongeza mabao mawili zaidi katika dakika za 54 na 89.
    Karim Benzema pia alifunga mabao mawili katika dakika za 52 na 56, wakati mabao mengine Gareth Bale alifunga moja, lililokuwa la kwanza Uwanja wa Santiago Bernabeu.
    Diego Mainz Garcia alijifunga kuipatia bao linguine Real dakika ya 83, wakati bao la kufutia machozi la Granada lilifungwa na Roberto Ibanez dakika ya 74.
    Kikosi cha Carlo Ancelotti sasa kinazidiwa pointi moja tu na vinara Barcelona katika msimamo wa La Liga, 68-67 ingawa Real wamecheza mechi moja zaidi (28-29). Barca watakuwa wageni wa Celta Vigo usiku wa leo.
    Kikosi cha Real Madrid kilikuwa; Casillas, Arbeloa, Ramos, Varane, Marcelo, Rodriguez/Jese dk61 Kroos/Illaramendi dk57, Modric, Bale, Benzema/Hernandez dk61 na Ronaldo.
    Granada: Oier, Foulquier, Mainz, Babin/Murillo dk61, Juan Carlos, Fran Rico/Silvestre dk57, Iturra, Ibanez, Rochina/Piti dk53, Candeias na El Arabi. 
    Ronaldo now has 24 La Liga hat-tricks - drawing level with Barcelona star Lionel Messi
    Cristiano Ronaldo akishangilia baada ya kuifungia mabao matano Real Madrid katika ushindi wa 9-1 leo

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-3026335/Real-Madrid-9-1-Granada-Cristiano-Ronaldo-nets-FIVE-Karim-Benzema-Gareth-Bale-score.html#ixzz3WRD18ghi 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RONALDO APIGA TANO REAL MADRID IKIIFUMUA GRANADA 9-1 LA LIGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top