• HABARI MPYA

    Thursday, October 31, 2013

    MAMBO YALIVYOKUWA TAIFA LEO BAADA YA POLISI KULIPUA MABOMU SIMBA NA KAGERA



    Moshi mweupe, baada ya Polisi kulipua mabobu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kufuatia vurugu zilizotokea katika mchezo baina ya Simba na Kagera.
    Polisi wakimsombasomba shabiki wa Simba baada ya kutokea vurugu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom TanzaniaBara baina ya timu hiyo na wageni Kagera Sugar ya Bukoba. Polisi walilazimika kurusha mabomu ya machozi kuwadhibiti mashabiki wa Simba SC waliokuwa wakivunja viti na kurusha uwanjani kwa kilichoonekana kukerwa na refa wa mchezo huo, Mohamed Theofile kuongeza dakika nne baada ya kutimia dakika 90 za kawaida, ambazo Kagera Sugar walizitumia kusawazisha bao na kupata sare ya 1-1. 

    Mtifuano, mashabiki wakikimbia kunusuru maisha yao

    Hatari tupu

    Kila mtu na roho yake

    Polisi na mashabiki wa Simba

    Jamaa anajisalimisha wakati mwenzake anakusanywa

    Polisi na mashabiki 

    Kipa wa Simba SC akizungumza na refa anayesindikizwa na refa

    Jukwaa la Orange namna viti vilivyonyofolewa

    Watu wamenyofoa viti vya kutosha

    Walivirusha uwanjani

    Viti zaidi

    Viti
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAMBO YALIVYOKUWA TAIFA LEO BAADA YA POLISI KULIPUA MABOMU SIMBA NA KAGERA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top