• HABARI MPYA

    Monday, July 29, 2013

    NEYMAR AFANYIWA VIPIMO LEO BARCA TAYARI KUANZA KAZI CAMP NOU

    IMEWEKWA JULAI 29, 2013 SAA 8:14 MCHANA
    MCHEZAJI aliyesajiliwa kwa Pauni Milioni 50, Neymar amefanyiwa vipimo vya afya mjini Barcelona tayari kwa mazoezi yake ya kwanza na klabu yake hiyo mpya.
    Barcelona itawapokea tena wachezaji wote waliokuwa kwenye Kombe la Mabara leo mcha, na Neymar atakuwa miongoni mwao pamoja na akina Xavi, Andres Iniesta, Cesc Fabregas na Lionel Messi.
    Itakuwa nafasi yake ya kwanza kujaribu kuwavutia wachezaji wenzake wapya baada ya kuweka rekodi ya kuwa mchezaji wa pili ghali katika klabu hiyo nyuma ya Zlatan Ibrahimovic aliyesajiliwa mwaka 2009 kwa Pauni Milioni 56.
    New kid on the block: Neymar during his routine pre-season medical at Barcelona
    Neymar akipimwa Barcelona
    Introductions: Gerardo Martino was giving his first training session with his whole squad
    Gerardo Martino alianza kazi ya kukinoa kikosi
     VIDEO  Gerardo Martino alvyoanza kazi Barcelona
      VIDEO  Neymar, Xavi, Iniesta na Fabregas wakifanyiwa vipimo

    Neymar aling'ara kikosini Brazil na kuiwezesha kutwaa Kombe la Mabara Juni mwaka huu akiwafunga wachezaji wenzake wengi wa Barca wanaounda kikosi cha Hispania.
    Mmoja wa wapinzani wake siku hiyo, Fabregas, bado anatakiwa na Manchester United na kocha David Moyes anatumai kumnasa kabla ya pazia la usajili kufungwa Septemba 2. 
    New signing: Neymar went to Barcelona in June to be shown around the club
    Neymar alikwenda Barcelona Juni kwa ajili ya kutambulishwa tu
    Centre of attention: He was also displayed to the fans at the Nou Camp
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: NEYMAR AFANYIWA VIPIMO LEO BARCA TAYARI KUANZA KAZI CAMP NOU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top