• HABARI MPYA

    Friday, July 26, 2013

    STARS MAZOEZINI NAMBOOLE, CHANONGO AMTESA LUHENDE HADI AVUTA JEZI, CHUJI MOTO CHINI

    IMEWEKWA JULAI 26, 2013 SAA 11:34 JIONI
    Safi Chuji; Kiungo wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Athumani Iddi 'Chuji' akimtoka Juma Luizio wakati wa mazoezi ya timu hiyo jioni hii Uwanja wa Mandela, Namboole, Kampala, Uganda, kujiandaa na mchezo wa kesho dhidi ya wenyeji, Uganda, The Cranes. Kushoto ni Kocha Mkuu, Mdenmark, Kim Poulsen na kulia kabisa ni kiungo Frank Domayo.


    Acha jezi wewe; Haruna Chanongo akimtoka David Luhende anayevuta jezi

    Chuji akituliza mpira pembeni ya John Bocco

    Yuko sawa; Juma Kaseja akidaka

    Erasto Nyoni akimtoka Mudathir Yahya

    Ally Mustafa 'Barthez' akidaka mpira aliopigiwa  na kocha wa makipa, Juma Pondamali kulia, huku Juma Kaseja nyuma yake akimuangalia. Mwingine ni Mwadini Ally. Makipa wote wako fiti. 

    Aggrey Morris akimiliki mpira

    Juma Luizio akikokota mpira pembeni ya Chuji

    Kesho watatukoma; Mrisho Ngassa akikumbatiana na Kevin Yondan

    Mwadini Ally akipangua mpira wa juu mbele ya Juma Kaseja 

    Upepo zaidi; Wachezaji wa Stars wakikimbia kuzunguka Uwanja wa Mandela

    Kesho mtalia; Bin Zubeiry katikati akiwa na makocha wa Uganda, Kocha Mkuu Mserbia, Milutin Sredojevic 'Micho' na Msaidizi wake, Mganda Sam Timbe katika baa iliyopo kwenye Uwanja wa Namboole. Uganda walianza mazoezi leo saa 8:30 wakawapisha Stars.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: STARS MAZOEZINI NAMBOOLE, CHANONGO AMTESA LUHENDE HADI AVUTA JEZI, CHUJI MOTO CHINI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top