Bao pekee la Mtibwa Sugar U20 ya kocha Awadh Juma limefungwa na mshambuliaji wake tegemeo, Athumani Makambo dakika ya 97 na kuzima ndoto ya Vijana wa Choke Abeid kubeba taji la kwanza la michuano hiyo.
Mapema katika mchezo wa kuwania nafasi ya tatu, Azam FC iliichapa Kagera Sugar 3-1 hapo hapo Azam Complex.
Mabao yote ya Azam FC ya kocha Mohamed Badru yamefungwa na Cyprian Kachwele dakika za 22, 27 na 45 na ushei, wakati la Kagera Sugar ya kocha Vincent Barnabas limefumgwa na Hussein Kombo dakika ya 90 na ushei.
0 comments:
Post a Comment