• HABARI MPYA

    Thursday, October 09, 2014

    ROONEY ATAKA KUVUNJA REKODI YA MABAO YA SIR BOBBY CHARLTON ENGLAND

    MSHAMBULIAJI Wayne Rooney anajiamini ataweka rekodi ya kuwa mchezaji aliyeifungia mabao mengi zaidi timu yake ya taifa, England kwa kuvunja rekodi iliyowekwa na Sir Bobby Charlton.
    Rooney anashika nafasi ya nne kwa kuifungia mabao mengi England 41, yakiwa matatu nyuma ya Jimmy Greaves, saba nyuma ya Gary Lineker na nane nyuma ya Charlton mwenye mabao 49.
    Rooney, ambaye ana umri wa miaka 28 tu, ndiye Nahodha wa kikosi cha timu hiyo kwa sasa ambacho kitamenyana na San Marino Uwanja wa Wembley usiku wa leo. "Ni wakati wangu sasa kuwapiku wote. Najihisi naweza kabisa kufanya hivyo. Hiyo itakuwa heshima kubwa,"amesema.

    Wayne Rooney anashika nafasi ya nne katika orodha ya wafungaji wa kihistoria wa mabao England na anaamini atavunja rekodi ya Charlton

    WAKALI WA MABAO WA KIHISTORIA ENGLAND

    Sir Bobby Charlton - Mabao 49 katika mechi 106
    Gary Lineker - Mabao 48 katika mechi 80
    Jimmy Greaves - Mabnao 44 katika mechi 57
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ROONEY ATAKA KUVUNJA REKODI YA MABAO YA SIR BOBBY CHARLTON ENGLAND Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top