• HABARI MPYA

    Wednesday, October 22, 2014

    AZAM FC YAWEKA REKODI ‘BABU KUBWA’ LIGI KUU

    Na Nagma Khalid, DAR ES SALAAM 
    AZAM FC mwishoni mwa wiki imetimiza mechi 38 bila kufungwa katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Prisons Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.
    Shukrani kwake, beki Aggrey Morris aliyefunga bao hilo pekee kipindi cha kwanza kwa mpira wa adhabu kutoka umbali wa mita 20 na Azam ikapanda kileleni mwa Ligi Kuu kwa mara ya kwanza msimu huu.
    Azam FC, sasa ina pointi 10 sawa na Mtibwa Sugar ya Morogoro, lakini timu ya Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa na famili yake ina wastani mzuri zaidi wa mabao ya kufunga na kufungwa.
    Kikosi cha Azam FC kilichocheza mechi ya 38 bila kufungwa Jumamosi mjini Mbeya

    Februari 23, mwaka 2013 ndipo Azam FC ilifungwa kwa mara ya mwisho katika Ligi Kuu, ilipolala 1-0 mbele ya Yanga SC- unazungumzia misimu miwili iliyopita.
    Msimu uliopita Azam FC imekuwa bingwa wa Ligi Kuu kwa mara ya kwanza, bila ya kupoteza mchezo hata mmoja na sasa inaingia kwenye Raundi ya tano ya msimu huu wa ligi hiyo, bila kupoteza mechi.
    Azam FC imeshinda mechi tatu na kutoa sare mbili, kati ya mechi hizo, mbili imecheza ugenini, zote Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya ambako ilivuna pointi nne, kwa sare ya 0-0 na Prisons na ushindi wa 1-0 na Mbeya City.
    Azam FC ilicheza mechi zake mbili za kwanza za Ligi Kuu nyumbani, Uwanja wa Azam Complex na kushinda 2-0 dhidi ya Ruvu Shooting na 3-1 dhidi ya Polisi Morogoro.
    Rekodi ya kucheza mechi 38 bila kupoteza ni ya kujivunia na kama ingekuwa imewekwa na timu ‘za wananchi’- basi ingekuwa ikiimbwa kila siku kwenye vyombo habari.
    Kocha Mcameroon, Joseph Marius Omog anataka kuendeleza rekodi hiyo kwa kuhakikisha kwamba na msimu huu pia, Azam FC inamaliza Ligi bila kupoteza mechi.

    AZAM FC MECHI 38 BILA KUFUNGWA LIGI KUU

    Feb 23, 2013: Yanga SC 1-0 Azam FC
    Machi 9, 2013:  Azam 1-1 Polisi Moro
    Machi 27, 2013: Azam 3-0 Prisons
    Machi 30, 2013: Ruvu Shooting 0-1 Azam FC
    Aprili 11, 2013: Azam 1-1 African Lyon
    Aprili 14, 2013: Azam FC 2-2 Simba
    Aprili 26, 2013: Coastal Union 1-1 Azam FC
    Mei 11, 2013:  Azam FC 3-0 JKT Mgambo
    Mei 18, 2013: JKT Oljoro 0-1 Azam FC
    Agosti 24, 2013: Mtibwa Sugar 1 – 1 Azam FC
    Agosti 28, 13: Rhino Rangers 0-2 Azam FC
    Sept 14, 2013: Kagera Sugar 1-1 Azam FC
    Sepe 18, 2013: Azam FC 1-1 Ashanti United
    Sept 22, 2013: Azam 3-2 Yanga SC 
    Sept 29, 2013: Prisons 1-1 Azam FC
    Mei 5, 2013:   Coastal Union 0-0 Azam FC
    Okt 9, 2013: Azam FC 2-0 JKT Mgambo
    Okt 13, 2013: Azam FC 3-0 JKT Ruvu Stars
    Okt 19, 2013: JKT Oljoro FC 0 – 1 Azam FC
    Okt 28, 2013: Simba SC 1-2 Azam FC
    Nov 2, 2013: Azam 3-0 Ruvu Shooting
    Nov 7, 2013: Azam 3-3 Mbeya City
    Nov 25, 2014: Azam 1-0 Mtibwa Sugar
    Nov 29, 2014: Azam 1- 0 Rhino Rangers
    Feb 2, 2014: Azam 4-0 Kagera Sugar
    Feb 23, 2014: Azam 2-2 Prisons
    Feb 26, 2014: Ashanti United 0-4 Azam
    Machi 15, 2014: Azam FC 4-0 Coastal Union
    Machi 19, 2014: Yanga SC 1-1 Azam FC
    Machi 23, 2014: Azam FC 1-0 JKT Oljoro FC
    Machi 26, 2014: JKT Mgambo 0-2 Azam FC
    Machi 30, 2014: Azam FC 2-1 Simba SC
    Aprili 10, 2014: Ruvu Shooting 0-3 Azam FC
    Aprili 13, 2014: Mbeya City 1-2 Azam FC
    Aprili 19, 2014: Ruvu Stars 0-1 Azam FC
    Sept 20, 2014: Azam FC 3-1 Polisi Moro
    Sept 27, 2014: Azam FC 2-0 Ruvu Shooting
    Okt  4, 2014: Prisons 0-0 Azam FC
    Okt 18, 2014: Mbeya City 0-1 Azam FC
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC YAWEKA REKODI ‘BABU KUBWA’ LIGI KUU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top