Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
SIMBA SC imefanya mazoezi kwa mara ya kwanza leo tangu sare ya 0-0 na mahasimu wao, Yanga SC Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Hata hivyo, wachezaji watatu, beki Joseph Owino, kiungo Shaaban Kisiga na mshambuliaji Emmanuel Okwi hawakufanya mazoezi jioni ya leo viwanja vya Chuo Kikuu, Dar es Salaam.
Kisiga aliomba udhuru, wakati Okwi aliomba ruhusa ya kumpeleka hospitali Mganda mwenzake, Owino akafanyiwe vipimo.
Kocha Mzambia, Patrick Phiri ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba wachezaji wote hao wana ruhusa yake ya kukosa mazoezi ya leo, lakini kesho watakuwepo.
“Wameomba ruhusa na shida zao tumezielewa, tumewakubalia, lakini kesho tutakuwa nao mazoezini,”amesema.
Simba SC baada ya sare nne za mechi zake zote za mwanzo za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Jumamosi itahamishia mawindo yake mjini Mbeya itakapokuwa mgeni wa Prisons.
SIMBA SC imefanya mazoezi kwa mara ya kwanza leo tangu sare ya 0-0 na mahasimu wao, Yanga SC Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Hata hivyo, wachezaji watatu, beki Joseph Owino, kiungo Shaaban Kisiga na mshambuliaji Emmanuel Okwi hawakufanya mazoezi jioni ya leo viwanja vya Chuo Kikuu, Dar es Salaam.
Kisiga aliomba udhuru, wakati Okwi aliomba ruhusa ya kumpeleka hospitali Mganda mwenzake, Owino akafanyiwe vipimo.
![]() |
Joseph Owino amesababisha Emmanue Okwi asiwepo mazoezini leo |
Kocha Mzambia, Patrick Phiri ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba wachezaji wote hao wana ruhusa yake ya kukosa mazoezi ya leo, lakini kesho watakuwepo.
“Wameomba ruhusa na shida zao tumezielewa, tumewakubalia, lakini kesho tutakuwa nao mazoezini,”amesema.
Simba SC baada ya sare nne za mechi zake zote za mwanzo za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Jumamosi itahamishia mawindo yake mjini Mbeya itakapokuwa mgeni wa Prisons.
0 comments:
Post a Comment