KLABU ya Chelsea itamenyana na Atletico Madrid katika Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Droo ya Nusu Fainali iliyofanyika leo imemtupa kocha Jose Mourinho kwa vinara wa Primera Division leaders, ambao wametoa Barcelona katika Robo Fainali.
Real Madrid itamenyana na mabingwa wateteziu, Bayern Munich katika Nusu Fainali nyingine huku mechi za kwanza zikichezwa Aprili 22 na 23 na marudiano wiki inayofuata.
Real Madrid itamenyana na mabingwa wateteziu, Bayern Munich katika Nusu Fainali nyingine huku mechi za kwanza zikichezwa Aprili 22 na 23 na marudiano wiki inayofuata.
Ikumbukwe kipa tegemeo wa Atletico Thibaut Courtois mwenye umri wa miaka 21 anachezea timu hiyo kwa mkopo kutoka Chelsea.
Tutakutana Nusu Fainali: Kipa tegemeo wa Atletico Madrid, Thibaut Courtois anaweza kukutana na klabu iliyomlea Chelsea katika Nusu Fainali
Kuna taarifa kwamba Chelsea imeiruhusu klabu hiyo ya Hispania kumchezesha kipa huyo Mbelgiji katika mechi zote za Nusu Fainali, kwa kulipa kiasi cha Euro Milioni 3 kwa kila mechi.
Pamoja na hayo, UEFA imepinga hilo ikisema ni kinyume cha sheria na imeweka wazi kwamba inatarajia kipa huyo wa kimataifa wa Ubelgiji atakuwa huru kucheza mechi zote dhidi ya The Blues bila masharti.
Kuna taarifa kwamba Chelsea imeiruhusu klabu hiyo ya Hispania kumchezesha kipa huyo Mbelgiji katika mechi zote za Nusu Fainali, kwa kulipa kiasi cha Euro Milioni 3 kwa kila mechi.
Pamoja na hayo, UEFA imepinga hilo ikisema ni kinyume cha sheria na imeweka wazi kwamba inatarajia kipa huyo wa kimataifa wa Ubelgiji atakuwa huru kucheza mechi zote dhidi ya The Blues bila masharti.
Anapanga droo: Nyota wa zamani wa Ureno, Luis Figo akiwa ameshika kadi ya droo yenye jina la Real Madrid
0 comments:
Post a Comment