• HABARI MPYA

    Friday, April 18, 2014

    AZAM VETERANS CHUPUCHUPU KWA ZANZIBAR VETERANS CHAMAZI, KAMA SIYO FATHER WANGELALA LEO

    BAO la dakika ya 75 la kiungo mtaalamu wa Azam Veterans, Nassor Idrissa Mohammed ‘Father’ jioni hii limeinusuru timu hiyo kuzama mbele ya Wazee Veterans ya Zanzibar baada ya kupata sare ya 3-3 katika mchezo wa kirafiki uliopigwa Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
    Nassor alifunga bao hilo kwa ufundi wa hali ya juu baada ya kazi nzuri ya Vivek Nagul aliyekuwa akicheza pamoja naye katika safu ya kiungo hii leo.
    Kali Ongala alifunga bao zuri kutoka katikati ya Uwanja
    Kikosi cha Azam Veterans kilichoanza
    Abdulkarim Amin 'Popat' akimuacha chini beki wa Zanzibar, huku Nassor Idrissa 'Father' akiwa tayari kutoa msaada
    Philipo Alando akimtoka beki wa Zanzibar Veterans
    Beki Iddi Cheche akiondoka na mpira baada ya kuzuia shambulizi la Wazanzibari

    Azam ilikwenda kupumzika ikiwa inaongoza kwa mabao 2-0, yaliyotiwa kimiani na Abdulkarim Amin ‘Popat’ dakika ya saba na Kally Ongalla dakika ya 30, lakini kipindi cha pili Wazee inayoundwa na wachezaji wa zamani wa kimataifa wa Zanzibar ilifanikiwa kusawazisha ndani ya 13 za kipindi cha pili.
    Alianza Abdallah Matake Kassim dakika ya 49 na baadaye Mbaraka Nyangi dakika ya 57 ambaye pia alifunga bao la tatu dakika ya 64, kabla ya Father kuiepusha na aibu ya kufungwa nyumbani Azam Veterans.
    Bao tamu kuliko yote hii leo ni lile lililofungwa na Kali Ongala aliyefumua shuti kutoka katikati ya Uwanja. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM VETERANS CHUPUCHUPU KWA ZANZIBAR VETERANS CHAMAZI, KAMA SIYO FATHER WANGELALA LEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top