• HABARI MPYA

    Tuesday, April 29, 2014

    MAZEMBE NA AS VITA ZOTE ZA DRC ZAPANGWA KUNDI MOJA LIGI YA MABINGWA, NI VITA YA WEUSI MWAKA HUU

    Na Prince Akbar, Dar es Salaam
    WAWAKILISHI wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), TP Mazembe na AS Vita wamepangwa kundi moja, A katika Ligi ya Mabingwa Afrika kama ilivyo kwa Esperance na C.S Sfaxien za Tunisia ambazo zipo kundi B pamoja na E.S Setif ya Algeria na Ahly Benghazi ya Libya.
    Mabingwa mara tano wa michuano hiyo, Zamalek ya Misri wapo pia Kundi A  na wababe hao wa DRC na vigogo wa Sudan, Al Hilal. 
    Vijana wa kazi; Washambuliaji tegemeo wa TP Mazembe, Watanzania Mbwana Samatta kulia na Thomas Ulimwengu kushoto wamepangwa kundi moja na AS Vita ya DRC pia

    Mechi zinatarajiwa kuchezwa kuanzia kati ya Mei 16 na 18 na 23 na 25, Juni 6 na 8, Julai 25 na 27, Agosti 8 na 10 na  22 na 24 huku timu zitakazoshika nafasi mbili za juu kwenye makundi zikisonga Nusu Fainali.

    MAKUNDI LIGI YA MABINGWA AFRIKA:
    Kundi A: TP Mazembe (DRC), Al-Hilal (Sudan), Zamalek (Misri) na AS Vita (DRC)
    Kundi B: Esperance (Tunisia), CS Sfaxien (Tunisia),
    Entente Setif (Algeria) na Al-Ahly Benghazi (Libya).
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAZEMBE NA AS VITA ZOTE ZA DRC ZAPANGWA KUNDI MOJA LIGI YA MABINGWA, NI VITA YA WEUSI MWAKA HUU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top