MRISHO Khalfan Ngassa ‘Anko’ amekamilisha mechi tatu za makundi katika michuano ya kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge bila kufunga bao ‘hata la offside’.
Mshambuliaji huyo wa Yanga amecheza mechi ya tatu leo ya Kundi B na kutolewa dakika ya 81 akimpisha Ramadhani Singano ‘Messi’ akiwa hajapiga hata shuti moja langoni mwa Burundi, Stars ikishinda 1-0 zaidi ya mpira wa adhabu ambao haukuwa na madhara. Lakini Ngassa ndiye aliyetoa pasi ya bao la Stars leo lililofungwa na Mbwana Samatta dakika ya saba.
Hii ni mech ya pili mfululizo Ngassa anatolewa baada kutolewa pia katika mechi iliyopita dhidi ya Somalia, alipotolewa dakika 79 kumpisha Farid Mussa.
![]() |
| Ngassa akiwa benchi leo Uwanja wa Afraha baada ya kutolewa |
Mshambuliaji huyo wa Yanga amecheza mechi ya tatu leo ya Kundi B na kutolewa dakika ya 81 akimpisha Ramadhani Singano ‘Messi’ akiwa hajapiga hata shuti moja langoni mwa Burundi, Stars ikishinda 1-0 zaidi ya mpira wa adhabu ambao haukuwa na madhara. Lakini Ngassa ndiye aliyetoa pasi ya bao la Stars leo lililofungwa na Mbwana Samatta dakika ya saba.
Hii ni mech ya pili mfululizo Ngassa anatolewa baada kutolewa pia katika mechi iliyopita dhidi ya Somalia, alipotolewa dakika 79 kumpisha Farid Mussa.



.png)
0 comments:
Post a Comment