• HABARI MPYA

    Thursday, October 15, 2015

    KIIGINILIO YANGA SC NA AZAM FC SH 5,000 KWA WALALAHOI, KWA 'WASHUA' 30,000

    SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limetangaza viingilio vya mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom siku ya Jumamosi kati ya Yanga SC dhidi ya Azam utakaochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, kiingilio vha chini kikiwa ni shilingi elfu tano (5,000) kwa viti vyenye rangi ya bluu, Kijani na Machungwa.
    Tiketi za mchezo huo zitauzwa siku ya mchezo Jumamosi katika eneo la Uwanaj wa Taifa jijini Dar es salaam, ambapo kingilio cha juu kitakua ni Shilingi Elfu Thelathini (30,000) kwa VIP A, na Shilingi Elfu Ishirini (20,000) kwa VIP B & C.
    Mwamuzi wa mchezo huo atakua Abdallah Kambuzi kutoka mkoani Shinyanga, akisaidiwa na Makame Mdogo (Shinyanga), Robert Luhemeja (Mara), mwamuzi wa akiba Frank Komba (Dsm) huku Kamisaa wa mchezo akiwa Joseph Mapunda kutoka mkoa wa Ruvuma.
    Shomary Kapombe wa Azam FC akibinuka tik tak kuokoa bao la wazii katika mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga SC. 

    Michezo mingine ya Ligi Kuu ya Vodacom siku ya Jumamosi ni Majimaji FC dhidi ya African Sports katika uwanja wa Majimaji mjini Songea, Ndanda FC wakiwakaribisha Toto African katika dimba la Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.
    Mbeya City FC watawakaribisha Simba SC kwenye dimba la uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, Stand United wakiwakaribisha Tanzania Prisons kwenye uwanja wa Kambarage mjini Shinyaga, Jijini Tanga Coastal Union watakua wenyeji wa Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Mkwakwani.
    Jumapili ligi hiyo itaendelea kwa michezo miwili, Maafande wa Mgambo Shooting watakua wenyeji wa Kagera Sugar uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, huku wachimba Almasi wa Mwadui FC wakiwakaribisha JKT Ruvu katika uwanja wa Mwadui Complex.
    Wakati huo huo: Ligi Daraja la Kwanza chini (FDL) inatarajiwa kuendelea wikiendi hii kwa michezo 12 kuchezwa katika viwanja mbalimbali kutoka katika makundi yote matatu ya A, B, na C.
    Ijumaaa African Lyon watakuwa wenyeji wa Polisi Dodoma katika uwanja wa Karume jijini Dar es salaam, ukiwa ni mchezo wa kundi A.
    Jumamosi Kundi A, Mjii Mkuu (CDA) watakua wenyeji wa Kiluvya Uinted katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma, KMC wakiwakaribisha Polisi Dar kwenye uwanja wa Karume jijini Dar es salaam.
    Kundi B, Kimondo FC watawakaribisha Polisi Morogoro uwanja wa Vwawa – Mbozi, Burkinafaso dhidi ya Kurugenzi uwanja wa Jamhuri Morogoro, Njombe Mji dhidi ya JKT Mlale uwanja Amani Njombe.
    Kundi C, Mbao FC dhidi ya Panone FC uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, Rhino Rangers dhidi ya Polisi Mara uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Tabora, Geita Gold Vs Polisi Tabora uwanja wa Nyankumbu Geita na JKT Kanembwa Vs JKT Oljoro uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
    Ligi hiyo itaendelea siku ya Jumapili kwa michezo miwili kuchezwa, Ashanti United watawakaribsiha Friends Rangers uwanja wa Karume jijini Dar es salaam, huku Ruvu Shooting wakiwa wenyeji wa Lipuli FC katika uwanja wa Mabatini Mlandizi mkoani Pwani.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KIIGINILIO YANGA SC NA AZAM FC SH 5,000 KWA WALALAHOI, KWA 'WASHUA' 30,000 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top