WENYEJI, Chelsea wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Tottenham Hotspur jana katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Stamford Bridge Jijini London.
Mabao ya The Blues yamefungwa na washambuliaji, Muingereza mwenye asili ya Sierra Leon, Trevoh Chalobah dakika ya 24 na Msenegal, Nicolas Jackson dakika ya 72.
Kwa ushindi huo, Chelsea inafikisha pointi 51 na kusogea nafasi ya nane, wakati Tottenham Hotspur inabaki na pointi zake 60 nafasi ya tano baada ya wote kucheza mechi 34.
0 comments:
Post a Comment