// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); AZAM FC FC YASAJILI KIUNGO MPYA MCOLOMBIA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE AZAM FC FC YASAJILI KIUNGO MPYA MCOLOMBIA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Saturday, May 25, 2024

    AZAM FC FC YASAJILI KIUNGO MPYA MCOLOMBIA


    KLABU ya Azam FC imeendela kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu ujao baada ya kumtambulisha kiungo mpya, Ever Meza iliyemnunua kutoka klabu ya Leonnes ya kwao, Colombia.
    Meza, aliyezaliwa Julai 21, 2000; alikuwa kwa mkopo kwenye klabu ya Alianza FC ya huko huko Colombia, amesaini mkataba wa miaka minne utakaomuweka Azam Complex hadi mwaka 2028.
    Huyo anakuwa mchezaji mpya wa tatu kusainishwa mkataba Azam FC hata kabla ya dirisha la usajili kufunguliwa, baada ya beki wa kati, Yoro Mamadou Diaby kutoka Stade Malien pia ambako alikuwa anacheza kwa mkopo kutoka akademi ya Yeleen Olympique ya Mali na kiungo mshambuliaji, Muivory Coast, Franck Tiesse kutoka Stade Malien.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC FC YASAJILI KIUNGO MPYA MCOLOMBIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top