• HABARI MPYA

    Saturday, March 11, 2023

    TANZANIA PRISONS YAICHAPA NAMUNGO FC 3-2 RUANGWA


    TIMU ya Tanzania Prisons imeibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya wenyeji, Namungo FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara leo Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi.
    Mabao ya Tanzania Prisons yamefungwa na Samson Mbangula dakika ya 13, Edwin Balua dakika ya 28 na Jeremiah Juma dakika ya 52, wakati ya Namumgo FC yamefungwa na Hassan Kabunda dakika ya 78 na Relliant Lusajo dakika ya 86.
    Kwa ushindi huo, Tanzania Prisons inafikisha pointi 25 na kusogea nafasi ya 13, wakati Namungo FC inabaki na pointi zake 32 nafasi ya saba baada ya wote kucheza mechi 25.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TANZANIA PRISONS YAICHAPA NAMUNGO FC 3-2 RUANGWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top