WENYEJI, Liverpool FC wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Wolverhampton Wanderers katika mchezo wa Ligi Kuu ya England jana Uwanjanwa Anfield Jijini Liverpool.
Mabao ya Liverpool yamefungwa na beki Mholanzi, Virgil van Dijk dakika ya 73 na mshambuliaji Mmisri, Mohamed Salah dakika ya 77.
Kwa ushindi huo wanafikisha pointi 39 katika mchezo wa 24 na kusogea nafasi ya sita, wakati Wolves wanabaki na pointi zao 24 za mechi 25 nafasi ya 15.
0 comments:
Post a Comment