• HABARI MPYA

    Saturday, March 04, 2023

    DUCHU AIPELEKA MTIBWA SUGAR NANE BORA ASFC


    WENYEJI, Mtibwa Sugar wamefanikiwa kwenda Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya KMC leo Uwanja wa Manungu Complex, Turiani mkoani Morogoro.
    Bao pekee la Mtibwa Sugar leo limefungwa na beki wake wa kulia, David Kameta ‘Duchu’ kwa mkwaju wa penalti dakika ya 45 baada ya mlinzi wa KMC kuunawa mpira kwenye boksi.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: DUCHU AIPELEKA MTIBWA SUGAR NANE BORA ASFC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top