ALIYEKUWA kiungo wa Yanga SC, Balama Mapinduzi amejiunga na mabingwa wa zamani wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Mtibwa Sugar.
Pamoja na Mapinduzi, mchezaji wa zamani wa Mbao FC ya Mwanza, wengine wapya waliotambulishwa Mtibwa ni beki Mkongo, Paschal Kitenge kutoka Coastal Union ya Tanya.
Wengine ni kipa Mohamed Makaka kutoka Ruvu Shooting, winga Charles Ilamfya kutoka KMC na beki Iddi Mobby kutoka Polisi Tanzania.
0 comments:
Post a Comment