BONDIA Yussuf Changalawe amefanikiwa kuingia Nusu Fainali ya Ndondi kwenye Michezo ya Jumuiya ya Madola baada ya kumshinda kwa Knockout (KO) Lingelier wa St Lucia usiku wa jana katika pambano la uzito wa Light Heavy Jijini Birmingham nchini England.
Changalawe atakutana bondia wa Scotland katika nusu fainali, pambano ambalo akishinda atakuwa amejihakikishia Medali ama ya Dhahabu, au Fedha akishindwa ataondoka na Medali ya Shaba.
0 comments:
Post a Comment