MSHAMBULIAJI Robert Lewandowski jana amekuwa mchezaji wa tatu katika historia ya Bundesliga kufikisha mabao 250 baada ya Mpoland huyo kufunga mabao mawili Bayern Munich ikiichapa Wolfsburg 2-1, bao la wageni likifungwa na Maximilian Philipp.
Lewandowski aliyefunga mabao yake 74 ya awali Bundesliga akiwa na Borussia Dortmund, anaungana na gwiji wa Bayern, Gerd Muller na Klaus Fischer – nyota wa zamani wa Schalke – katika orodha ya wachezaji pekee waliofunga mabao 250 Bundesliga PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment