• HABARI MPYA

    Monday, December 14, 2020

    MAN UNITED NA REAL SOCIEDAD, ARSENAL NA BENFICA EUROPA LEAGUE


    Manchester United itamenyana na vinara wa LaLiga, Real Sociedad katika hatua ya 32 UEFA Europa League
     

    RATIBA KAMILI

    Wolfsberger AC vs Tottenham Hotspur

    Dynamo Kyiv vs Club Brugge

    Real Sociedad vs Manchester United

    Benfica vs Arsenal

    Crvena Zvezda vs AC Milan

    Royal Antwerp vs Rangers

    Slavia Prague vs Leicester City

    Salzburg vs Villarreal

    Braga vs Roma

    Krasnodar vs Dinamo Zagreb

    Young Boys vs Bayer Leverkusen

    Molde vs Hoffenheim

    Granada vs Napoli

    Maccabi Tel-Aviv vs Shakhtar Donetsk

    Lille vs Ajax

    Olympiacos vs PSV Eindhoven

    Mechi za kwanza zitachezwa Alhamisi ya Februari 18; marudiano Alhamisi ya Februari 25

    TIMU ya Manchester United itamenyana na vinara wa LaLiga, Real Sociedad katika hatua ya 32 UEFA Europa League.
    Baada ya kuangukia kwenye michuano hiyo kufuatia kutolewa katika Ligi ya Mabingwa, kocha Ole Gunnar Solskjaer atakabiliwa na matihani mwingine mgumu mbele ya timu inayoongoza kwa kufunga mabao kwenye Ligi Kuu ya Hispania kwa sasa.
    Arsenal nay imeoangiwa mpinzani mgumu katika Hatua hii, ambayo ni Benfica ya Ureno huo ukiwa mtihani mwingine kwa kocha Mikel Arteta kufuatia matokeo mabaya mfululizo msimu huu.
    Kocha maarufu, Mreno Jose Mourinho kidogo hatakuwa na kazi ngumu baada ya Tottenham Hotspur kupangiwa Wolfsberger ya Austria.
    Mechi ya Tottenha itachezwa Saa 24 kabla ya nyingine Jumatano ya Februari 24, kwa sababu Arsena watakuwa wana mechi pia, hivyo Jiji la London haliwezi kuwa na michezo miwili ya Europa League wakati mmoja.
    Leicester City ni timu nyingine iliyopata mpinzani mwepesi kidogo, kwani itamenyana na Slavia Prague.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN UNITED NA REAL SOCIEDAD, ARSENAL NA BENFICA EUROPA LEAGUE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top