• HABARI MPYA

    Monday, December 14, 2020

    BARCA NA PSG, RONALDO ARUDISHWA URENO 16 BORA LIGI YA MABINGWA

    MABINGWA watetezi, Bayern Munich watamenyana na Lazio ya Italia katika Hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya mwakani.
    Chelsea itamenyana na Atletico Madrid, wakati Liverpool wataivaa RB Leipzig na Manchester City itacheza na Borussia Monchengladbach.
    Barcelona ya Lionel Messi itamenyana na Paris Saint-Germain ya Neyamr, wakati Cristiano Ronaldo ataiongoza Juventus dhidi ya Porto ya nyumbani kwao, Ureno.
    Lionel Messi (kulia) ataiongoza Barcelona dhidi ya PSG iliyofika fainali na kufungwa na Bayer Munich msimu uliopita 

    Mechi nyingine za hatua hiyo Sevilla itamenyana na Borussia Dortmund, wakati mabingwa mara 13, Real Madrid watamenyana na Atalanta.

    Mechi za kwanza zitachezwa na kati ya Februari 16, 17 na 23 na 24 , na za marudiano zitachezwa kati yaMachi 9 na 10 na 16 na 17 mwakani, 2021.
    RATIBA KAMILI
    Gladbach v Man City
    Lazio v Bayern
    Atletico v Chelsea
    Leipzig v Liverpool
    Porto v Juventus
    Barcelona v PSG
    Sevilla v Dortmund
    Atalanta v Real Madrid
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BARCA NA PSG, RONALDO ARUDISHWA URENO 16 BORA LIGI YA MABINGWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top