• HABARI MPYA

    Thursday, December 31, 2020

    REAL MADRID YALAZIMISHWA SARE 1-1 NA ELCHE KATIKA LA LIGA


    REAL Madrid imelazimishwa sare ya 1-1 na wenyeji, Elche katika mchezo wa La Liga Uwanja wa Manuel Martinez Valero usiku wa jana.
    Luka Modric alianza kuifungia Real Madrid dakika ya 20, lakini Fidel Chaves akaisawazishia Elche kwa penalti dakika ya 52 baada ya Dani Carvajal kumvuta jezi Antonio Barragan. 
    Matokeo hayo yanaifanya Real Madrid ifikishe pointi 33 baada ya kucheza mechi 16 na wanabaki nafasi ya pili, wakizidiwa pointi mbili na mahasimu wao, Atletico Madrid ambao pia wana mechi mbili mkononi 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: REAL MADRID YALAZIMISHWA SARE 1-1 NA ELCHE KATIKA LA LIGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top