• HABARI MPYA

    Saturday, September 26, 2015

    MAN CITY ‘YACHEZEA’ 4-1 KWA SPURS ENGLAND

    TIMU ya Manchester City imepoteza mchezo wa pili katika Ligi Kuu ya England msimu huu kufuatia kipigo cha mabao 4-1 kutoka Tottenham Hotspurt Uwanja wa White Hart Lane
    City ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 25 kupitia kwa Kevin De Bruyne, kabla ya Eric Dier kusawazisha dakika ya 45.
    Toby Alderweireld akaifungia bao la pili Spursdakika ya 50 kabla ya Harry Kane kufunga la tatu dakika ya 61 na Erik Lamela la nne dakika ua 79.
    Kikosi cha Tottenham kilikuwa; Lloris, Walker, Alderweireld, Vertonghen, Davies, Dier, Alli, Lamela/Carroll dk87, Son Heung-min/N'Jie dk75, Eriksen/Chadli dk68 na Kane.
    Manchester City; Caballero, Sagna, Demichelis, Otamendi, Kolarov, Fernandinho/Nasri dk69, Fernando, De Bruyne, Toure/Jesus Navas dk56, Sterling na Aguero/Roberts dk86.
    Mshambuliaji wa Tottenham, Harry Kane akishangilia baada ya kufunga dhidi ya Manchester City leo PICHA ZAIDI GONGA HAPA
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN CITY ‘YACHEZEA’ 4-1 KWA SPURS ENGLAND Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top