• HABARI MPYA

    Tuesday, September 22, 2015

    AZAM FC WAREJEA DAR KUISUBIRI MBEYA CITY, PATASHIKA LITAKUWA CHAMAZI JUMAPILI HII

    MECHI ZIJAZO LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA
    Jumamosi Septemba 26, 2015
    Simba SC Vs Yanga SC
    Coastal Union Vs Mwadui FC
    Prisons FC Vs Mgambo JKT
    JKT Ruvu Vs Stand United
    Mtibwa Sugar Vs Majimaji FC
    Kagera Sugar Vs Toto Africans
    Septemba 27, 2015
    African Sports Vs Ndanda FC
    Azam FC Vs Mbeya City 
    Azam FC watakuwa wenyeji wa Mbeya City katika mchezo ujao wa Ligi Kuu 

    Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM
    AZAM FC imerejea jana usiku Dar es Salaam kutoka Shinyanga ambako ilifanikiwa kuvuna pointi sita katika mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
    Baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Stand United na 1-0 dhidi ya Mwadui FC, Azam FC imetua kwa ndege usiku wa jana Dar es Salaam kwa maandalizi ya mchezo ujao dhidi ya Mbeya City.
    Mabingwa hao wa Afrika Mashariki na Kati watakuwa wenyeji wa Mbeya City katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
    Azam FC imeshinda mechi zote tatu za mwanzo za Ligi Kuu, dhidi ya Prisons 2-1 Chamazi na hizo za Shinyanga, ikiwa inababana mbavu na vigogo, Simba na Yanga SC kileleni.
    Mechi za Azam FC inayodhaminiwa na benki ya NMB na Mbeya City inayodhaminiwa na RB Battery za Bin Slum Company Limited, zimekuwa kali na za kusisimua popote zinapokutana timu hizo, iwe Mbeya au Chamazi na Jumapili inatarajiwa patashika nyingine.

    MSIMAMO WA LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA BARA
    # TimuPWDLFADPtsMechi zilizopita 
    1Previous rank: 16330091+89WWW
    2Previous rank: 12330061+59WWW
    3Previous rank: 2330051+49WWW
    4Previous rank: 8330052+39WWW
    5Previous rank: 6320121+16LWW
    6Previous rank: 10311133+04LWD
    7Previous rank: 15311122+04DLW
    8Previous rank: 4311123-14WLD
    9Previous rank: 7310232+13LWL
    10Previous rank: 9310222+03LWL
    11Previous rank: 13310223-13WLL
    12Previous rank: 5310224-23LLW
    13Previous rank: 14310225-33WLL
    14Previous rank: 3301203-31DLL
    15Previous rank: 1300305-50LLL
    16Previous rank: 11300318-70LLL
    Ligi Kuu inayoonyeshwa moja kwa moja na Azam TV itaendelea Jumamosi ya Septemba 26 kwa mchezo kati ya mahasimu Simba SC na Yanga SC Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Coastal Union na Mwadui FC Uwanja wa Mkwakwani, Tanga, Prisons FC na Mgambo JKT Uwanja wa Sokoine, Mbeya, JKT Ruvu na Stand United Uwanja wa Karume, Dar es Salaam, Mtibwa Sugar na Majimaji FC Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro, Kagera Sugar na Toto Africans wakati Jumapili African Sports watakuwa wenyeji wa Ndanda FC Mkwakwani na Azam FC na Mbeya City Chamazi. 
    Baada ya raundi tatu za awali, mabingwa watetezi Yanga SC wanaongoza Ligi Kuu kwa wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa, kufuatia kufungana kwa pointi na Simba na Azam FC.  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC WAREJEA DAR KUISUBIRI MBEYA CITY, PATASHIKA LITAKUWA CHAMAZI JUMAPILI HII Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top