• HABARI MPYA

    Friday, March 03, 2023

    GEITA GOLD YATINGA ROBO FAINALI AZAM FEDERATION CUP


    WENYEJI, Geita Gold wamefanikiwa kwenda Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) baada ya ushindi wa 3-1 dhidi ya Green Warriors leo Uwanja wa Nyankumbu mjini Geita.
    Mabao ya Geita Gold yamefungwa na Manyasi dakika ya saba, Daniel Lyanga dakika ya 17 na Elias Maguli dakika ya 57, wakati la Green Warriors limefungwa na Thabit Thabit dakika ya tisa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: GEITA GOLD YATINGA ROBO FAINALI AZAM FEDERATION CUP Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top