MSHAMBULIAJI mpya. Mnorway Erling Haaland jana amefunga mabao matatu katika ushindi wa 6-0 wa Manchester City dhidi ya
Nottingham Forest kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Etihad.
Mabao hayo aliyofunga dakika za 12, 23 na 38 yanamfanya afikishe hat-trick mbili ndani ya mechi tano za mwanzo za msimu na ni ya pili mfululizo.
Mabao mengine ya Man City yamefungwa na Joao Cancelo dakika ya 50 na Julian Alvarez mawili dakika ya 65 na 87.
0 comments:
Post a Comment