• HABARI MPYA

    Wednesday, December 12, 2018

    YANGA KUANZA NA IHEFU AU TUKUYU STARS, AZAM NA MADINI AU STAND BABATI, SIMBA SC NA MASHUJAA KOMBE LA TFF

    RATIBA KAMILI AZAM SPORTS FEDERATION CUP 
    Namungo FC v Sahare All Stars/Deportivo
    Geita Electrict/Kamuyange v Kagera Sugar
    Mtibwa Sugar v Kiluvya United
    Lipuli FC v Laela FC/Mitumba FC  
    Stand United v Ashanti United
    Changanyikeni/Barger FC v Coastal Union
    Reha FC v Zakhem/Mkamba Rangers
    Maji Maji FC v Toto Africans/Gipco
    Boma FC v Njombe Mji FC
    Pan African /Villa Squad v Mwadui FC
    Cosmopolitan v Green Warriors 
    Rhino Rangers v Nyamongo FC/Bulyanhulu FC
    Azam FC v Madini FC/Stand Babati
    KMC v Tanzania Prisons
    Kilimanjaro Forest /Kilimanjaro Heroes v Polisi Tanzania
    Moro Kids/Maji Maji Rangers v Mbeya Kwanza 
    Geita Gold FC v Biashara United 
    Ruvu Shooting v Mucoba FC/Might Elephant 
    Yanga SC v Ihefu FC/Tukuyu Stars
    Singida United v Arusha FC 
    Sharp Striker/Usalama v Friends Rangers 
    Dodoma FC v Kasulu Stars/Home Boys
    Mufindi United v Alliance FC
    Mbeya City v Mgambo Shooting 
    African Lyon v Arusha United 
    Simba SC v Mashujaa FC (Kigoma) 
    La Familia/Area C v Mawenzi Market 
    Mbao FC v Dar City 
    Stand Dortmund/Milambo FC v JKT Tanzania  
    Mtwivila/Livingston v Pamba FC 
    Ndanda FC v Trans Camp
    Mnale FC v Kitayose/African Sports
    (Mechi zitachezwa kuanzia Desemba 21 hadi 24, 2018)
    Mtibwa Sugar iliifunga Singida United 3-2 na kutwaa taji la Azam Sports Federation Cup Juni 2, mwaka huu Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha  

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    VIGOGO, Azam, Simba na Yanga wote wataanzia nyumbani hatua ya 64 Bora ya michuano ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ijulikanayo kama Azam Sports Federation Cup (ASFC).
    Hiyo ni baada ya droo ya raundi ya tatu ya michuano hiyo, iliyofanyika leo makao makuu ya Azam TV, hapa Tabata, Dar es Salaam ikishuhudiwa KMC NA Tanzania Prisons kuibuka mchezo pekee utakaokutanisha wapinzani wa Ligi Kuu watupu.
    Azam FC watakuwa wenyeji wa ama Madini FC ya Arusha, au Stand ya Babati, Yanga SC wataikaribisha amaIhefu FC au Tukuyu Stars, zote za Mbeya na Simba SC watawaalika Mashujaa FC kutoka mkoani Kigoma.
    Mabingwa watetezi, Mtibwa Sugar wao wataanza na Mtibwa Sugar na Kiluvya United ya Pwani Uwanja wa Manungu, Turiani mkoani Morogoro, wakati washindi wa pili Singida United wataanzia nyumbani pia Uwanja wa Namfua mkoani Singida dhidi ya Arusha FC. 
    Mechi zitachezwa wikiendi ijayo kuanzia Desemba 21 hadi 24 na hii moja kwa moja inamaanisha mechi itachezwa kabla au baada ya mchezo wa marudiano wa Simba na Nkana Desemba 23 Dar es Salaam, lakini mabingwa wa Tanzania Bara wanajivunia kikosi kipana.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA KUANZA NA IHEFU AU TUKUYU STARS, AZAM NA MADINI AU STAND BABATI, SIMBA SC NA MASHUJAA KOMBE LA TFF Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top