Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
AZAM FC na Mtibwa Sugar zinaendelea kukabana kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, sasa zote zikiwa na pointi 10 kila moja, baada ya kucheza mechi nne.
Baada ya Mtibwa Sugar kutoka sare ya 0-0 na Polisi Uwanja wa Jamhuri, Morogoro ushindi wa 1-0 wa Azam FC dhidi ya Mbeya City umewapandisha kileleni mabingwa hao watetezi.
Azam FC sasa wanaongoza Ligi Kuu kwa wastani wao mzuri wa mabao- licha ya kulingana kwa pointi na Mtibwa.
Baada ya Mtibwa Sugar kutoka sare ya 0-0 na Polisi Uwanja wa Jamhuri, Morogoro ushindi wa 1-0 wa Azam FC dhidi ya Mbeya City umewapandisha kileleni mabingwa hao watetezi.
Azam FC sasa wanaongoza Ligi Kuu kwa wastani wao mzuri wa mabao- licha ya kulingana kwa pointi na Mtibwa.
Mechi nyingine za leo, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, watani wa jadi, Simba na Yanga wametoka sare ya 0-0 wakati Ndanda FC imefungwa nyumbani mabao 3-1 na Ruvu Shooting Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara.
Coastal Union imeichapa 2-0 Mgambo JKT mabao ya Rama Salim dakika ya 29 na Kenneth Masumbuko dakika ya 89.
Ligi Kuu itaendelea kesho kwa mchezo kati ya JKT Ruvu na wenyeji Prisons Uwanja wa Sokoine, Mbeya.
Coastal Union imeichapa 2-0 Mgambo JKT mabao ya Rama Salim dakika ya 29 na Kenneth Masumbuko dakika ya 89.
Ligi Kuu itaendelea kesho kwa mchezo kati ya JKT Ruvu na wenyeji Prisons Uwanja wa Sokoine, Mbeya.
0 comments:
Post a Comment