BAO pekee la Brian Umony kwa penalti limeipa KCC ya Uganda ushindi wa 1-0 dhidi ya Atletico ya Burundi katika mchezo wa Kundi B, Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, au Kombe la Kagame Uwanja wa Nyamirambo, Kigali, Rwanda.
Mshambuliaji huyo aliyetemwa Azam FC mwishoni msimu, sasa anatimiza mabao mawili katika mashindano haya ndani ya mechi tatu na sasa anaingia kwenye mbio za ufungaji bora dhidi ya mshambuliaji wa timu yake ya zamani, John Bocco ‘Adebayor’.
KCC inatimiza pointi sita baada ya mechi tatu, ikishinda mbili na kufungwa moja, hivyo kujiwekea asilimia kubwa ya kwenda Robo Fainali ya michuano hiyo.
APR yenye pointi tatu za mechi moja, inashuka dimbani mida hii kumenyana na Telecom ya Djibouti ambayo iliifunga KCC katika mchezo uliopita 2-1.
Mshambuliaji huyo aliyetemwa Azam FC mwishoni msimu, sasa anatimiza mabao mawili katika mashindano haya ndani ya mechi tatu na sasa anaingia kwenye mbio za ufungaji bora dhidi ya mshambuliaji wa timu yake ya zamani, John Bocco ‘Adebayor’.
![]() |
Brian Umony kushoto ameifungia KCC leo bao pekee la ushindi |
KCC inatimiza pointi sita baada ya mechi tatu, ikishinda mbili na kufungwa moja, hivyo kujiwekea asilimia kubwa ya kwenda Robo Fainali ya michuano hiyo.
APR yenye pointi tatu za mechi moja, inashuka dimbani mida hii kumenyana na Telecom ya Djibouti ambayo iliifunga KCC katika mchezo uliopita 2-1.
0 comments:
Post a Comment