• HABARI MPYA

    Friday, February 07, 2014

    YANGA WATAKIWA KUJITOKEZA KWA WINGI TAIFA KESHO, WAASWA SOKA YA COMORO IMEBADILIKA WAENDE KUISAPOTI TIMU ISHINDE

    Na Prince Akbar, Dar es Salaam
    MWENYEKITI wa Kamati ya Mashindano ya Kimataifa ya klabu ya Yanga SC ya Dar es Salaam, Seif Ahmed ‘Magari’ amewataka wapenzi na mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati mechi dhidi ya Komorozine ya Comoro.
    Yanga SC itamenyana na timu hiyo kesho kuanzia Saa 10:00 jioni katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Seif Magari amesema wana Yanga hawapaswi kuidharau timu hiyo kwa kuwa soka ya Comoro hivi sasa imebadilika.
    Weweee, soka ya Comoro imebadilika; Seif amewataka mashabiki wa Yanga kujitokeza kwa wingi kesho kuishangilia timu yao dhidi ya Komorozine

    Magari amesema wanatarajia upinzani mkubwa katika mchezo wa kesho, hivyo ni vyema mashabiki wakajitokeza kwa wingi kuwahamasisha wachezaji.“Unajua wataalamu wanasema shabiki ni mchezaji wa 12, sasa lazima wana Yanga waje kwa wingi kesho kuishangilia timu mwanzo hadi mwisho ili kuwapa nguvu wachezaji.
    “Mimi ninakuambia soka ya Comoro hivi sasa imebadilika, siyo kama enzi zile tunawafunga nyingi nyingi, hawa jamaa hivi sasa wamebadilika mno na sisi hatuidharau hii mechi hata kidogo,”amesema Seif Magari jioni hii alipozungumza na BIN ZUBEIRY.
    Mmiliki wa hoteli ya Sapphire Court, Kariakoo, Dar es Salaam walipofikia Komorozine, Abdulfatah Salim Saleh pia amewaasa Yanga kuitilia mkazo mechi ya kesho kwa sababu wapinzani wao wanaonekana kupania mno.
    “Hawa jamaa hapa wanaonekana wamepania sana na wako makini sana, sasa kama Yanga watadharau mechi shauri yao,”amesema Abdulfatah.   
    Katika kuonyesha kwamba Yanga inatilia mkazo mchezo huo, imekuwa kambini Bagamoyo mkoani Pwani tangu imerejea kutoka Uturuki, Januari 24, mwaka huu ilipokwenda kuweka kambi ya wiki mbili.
    Mjitokeze kwa wingi kesho; Mashabiki wa Yanga wametakiwa kumiminika Taifa kesho kuisapoti timu yao
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA WATAKIWA KUJITOKEZA KWA WINGI TAIFA KESHO, WAASWA SOKA YA COMORO IMEBADILIKA WAENDE KUISAPOTI TIMU ISHINDE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top