• HABARI MPYA

    Saturday, February 22, 2014

    HATIMAYE ROONEY AJITIA PINGU MVUA TANO MAN UNITED, SASA NDIYE MCHEZAJI ANAYELIPWA ZAIDI DUNIA NZIMA

    MSHAMBULIAJI Wayne Rooney amemshukuru kocha David Moyes jana usiku baada ya kujihakikishia mustakabali wake katika klabu ya Manchester United, kufuatia kusaini Mkataba mpya wa miaka mitano ambao utamfanya apate mshahara wa Pauni 300,000 kwa wiki.
    Rooney aliwaambia United alitaka kuondoka mwishoni mwa msimu uliopita baada ya kutofautiana na aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Sir Alex Ferguson na mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England walilazimika kupambana na ofa ya dau la Pauni Milioni 30 kutoka Chelsea.

    Rasmi: Rooney amethibitisha kusaini kwake Mkataba mpya United kwa kuandika kwenye ukurasa wake wa Facebook akisema 'furaha sana'Sorted: Rooney (centre) with executive vice chairman Ed Woodward and manager David Moyes
    Wa hapa hapa: Rooney (katikati) akiwa na Makamu Mwenyekiti wa klabu, Ed Woodward na kocha David Moyes jana baada ya kusaini Mkataba mpya
    Moyes alisema jana namna ambavyo alimshawishi mshambuliaji huyo wa kimataifa wa England kubaki Old Trafforf alipokutana naye katika kikao chake cha siri kilichofanyika Juni mwaka jana.

    MALIPO MAPYA YA ROONEY

    Pauni 15,600,000 kwa mwaka
    Pauni 300,000 kwa wiki
    Pauni 43,000 kwa siku
    Pauni 1,800 kwa saa
    Pauni 30 kwa dakika
    50p kwa sekunde
    Na Rooney ametoa shukrani zake kwa kocha wake huyo aliyemuibua Everton baada ya kusaini Mkataba ambao utamalizika Juni mwaka 2019 ambao unamfanya awe mchezaji anayelipwa zaidi duniani.
    Alisema: "Kulikuwa kuna tetesi kibao wakati wa majira ya joto, lakini nilitulia wakati David Moyes alipokuja kwenye klabu.
    "Nimekuwa na uhusiano mzuri naye na anaonyesha imani kubwa kwangu. Mazungumzo yamekuwa yakiendelea kwa muda mrefu – Nina furaha kusaini sasa.
    "Hii ni moja ya klabu kubwa duniani na fahamu kwamba nitacheza hapa kwa sehemu kubwa ya maisha yangu ya soka, ni kitu ambacho nasonga mbele kwa ajili hiyo. Nina furaha kwamba kila kitu sasa kimemalizwa na ninaweza kuelekeza fikra zangu kwenye soka yangu,"alisema.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: HATIMAYE ROONEY AJITIA PINGU MVUA TANO MAN UNITED, SASA NDIYE MCHEZAJI ANAYELIPWA ZAIDI DUNIA NZIMA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top