• HABARI MPYA

    Saturday, February 22, 2014

    REAL MADRID YAREJEA KILELENI LA LIGA, BALE AFUNGA BAO LA MSIMU

    WINGA Gareth Bale amefunga moja ya mabao bora ya msimu La Liga, Real Madrid ikiilaza mabao 3-0 Elche usiku huu.
    Nyota huyo wa zamani wa Tottenham alifunga bao hilo dakika ya 72 akimtungua kipa wa Elche, Manu Herrera. Mabao mengine ya Real yalifungwa na Illarramendi dakika ya 34 na Isco dakika ya 81.
    Real sasa inatimiza pointi 63 baada ya mechi 25 na kupanda kileleni, ikiishusha Barcelona yenye pointi 60 za mechi 24 katika nafasi ya pili. Cristiano Ronaldo hakucheza. 
    Bonge la bao: Gareth Bale (kulia) akisherehekea na wenzake baada ua kufunga bao tamu Uwanja wa Bernabeu leo
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: REAL MADRID YAREJEA KILELENI LA LIGA, BALE AFUNGA BAO LA MSIMU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top