Prisons jana iliifunga mabao 6-0 JKT Ruvu katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya. Mbadilisha matokeo kwenye bango la matokeo Uwanja wa Sokoine jana alifanya kazi yake vizuri, ilikuwa kila bao likifungwa anaweka kibao kinacholingana na idadi ya mabao, lakini kufika bao la sita akatafuta kibao namba 6 hakipo na kwa fikra za haraka akaona bora aongeze kibao namba moja mbele ya tano kupata mabao sita, lakini ikawa inasomeka 51-0. |
0 comments:
Post a Comment