• HABARI MPYA

    Thursday, February 06, 2014

    PICHA KAMILI SIMBA NA MTIBWA JAMHURI, HANS POPPE NA MAESTRO KAMA 'WAMEPIGWA SHOTI'

    Vita ya mabeki; Beki wa kushoto wa Simba SC, Issa Rashid 'Baba Ubaya' akigombera mpira na beki wa kulia wa Mtibwa Sugar, Hassan Ramadhani katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya jana Uwanja wa Jamhuri, Morogoro ambao ulimalizika kwa sare ya 1-1.
    Rmadhani Singano 'Messi' wa Simba SC akitafuta mbinu za kumtoka beki wa Mtibwa Sugar, Hassan Ramadhani
    Messi na Hassan
    Messi akipambana kuwatoka mabeki wa Mtibwa Sugar
    Mshambuliaji wa Simba SC, Ali Badru akiwatoka mabeki wa Mtibwa Sugar
    Kocha wa Mtibwa Sugar, Meck Mexime aliyeipa mgongo kamera akimtuliza Nahodha wake, Shaaban Nditi baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu kwenye mchezo huo
    Beki wa Mtibwa Sugar, Juma Mpakala kushoto akipambana na mshambuliaji wa Simba SC, Ali Badru
    Haroun Chanongo wa Simba SC kulia akigombea mpira na Jamal Mnyate wa Mtibwa Sugar
    Mshambuliaji wa Simba SC, Amisi Tambwe akimtoka beki wa Mtibwa Sugar, Salvatory Ntebe, huku Messi akiwa tayari kutoa msaada
    Kiungo wa Simba SC, Jonas Mkude akimtoka kiungo wa Mtibwa Shaaban Kisiga
    Mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Juma Luizio akipasua katikati ya wachezaji wa Simba SC, Haroun Chanongo kulia na Jonas Mkude kushoto
    11 walioanza Mtibwa Sugar leo
    11 wa Simba SC walioanza leo
    Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera kulia akiwasalimi wachezaji wa Simba SC kabla ya mechi. Hapa amepeana mikono na beki Joseph Owino. Katikati ni Messi na kushoto Donald Mosoti
    Wakubwa; Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe kulia ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili na Ibrahim Masoud 'Maestro' wakifuatilia mchezo huo
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: PICHA KAMILI SIMBA NA MTIBWA JAMHURI, HANS POPPE NA MAESTRO KAMA 'WAMEPIGWA SHOTI' Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top