| Hivi huyu Ndemla ana mkataba kweli Simba? Kigogo wa masuala ya Usajili ya klabu ya Yanga, Seif Ahmed Magari 'Tishio la Jiji' kulia akijadiliana jambo na Kocha wa zamani wa klabu hiyo, ambaye kwa sasa ni Mwandishi wa makala za michezo na mchambuzi wa mechi, Kenny Mwaisabula kushoto wakati wa mechi ya timu za vijana chini ya umri wa miaka 20 za Simba na JKT Oljoro jioni ya leo Uwanja wa Karume, Dar es Salaam. Seif alionekana kuvutiwa sana na uwezo wa wachezaji wa Simba SC, akiwemo kiungo Said Ndemla, anayepasua katikati ya wachezaji wa Oljoro picha ya chini. |
0 comments:
Post a Comment