• HABARI MPYA

    Wednesday, December 06, 2017

    YANGA NA SIMBA WAPATA VIBONDE KOMBE LA AZAM SPORTS FEDERATION

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    MABINGWA watetezi, Simba SC watamenyana na Green Worriers, zote za Dar es Salaam katika mchezo wa Raundi ya Pili ya Kombe la Azam Sports Federation kati ya Desemba 20 na 25 mwaka huu Jijini.
    Mahasimu wao, Yanga watamenyana na Reha FC katika hatua hiyo inayoshirikisha jumla ya timu 64, wakati Azam FC watamenyana na Area C ya Dodoma Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.
    Katika droo iliyopangwa leo studio za Azam TV, Tabata mjini Dar es Salaam, ikiongozwa na wachezaji nyota wa zamani nchini, makipa Steven Nemes, Mwameja Mohammed, beki Kenneth Mkapa na mshambuliaji Bitta John, washindi wa pili wa msimu uliopita, Mbao FC watamenyana na Makanayagio FC ya Rukwa.
    Ruvu Shooting watakuwa wenyeji wa Madini FC, Abajalo wataikaribisha Tanzania Prisons, Njombe Mji wataikaribisha Mji Mkuu, Boda Boda FC ya Arusha watakuwa wenyeji wa Singida United na Mwadui FC wataikaribisha Pepsi FC.
    Gwiji wa soka nchini, Kenneth Pius Mkapa (kushoto) akionyesha karatasi inayomtambulisha mpinzani wa Yanga, Reha FC. Kulia ni gwiji mwingine, Bitta John aliyeichagua Yanga
    Makipa maarufu wa zamani, Mohammed Mwameja (kulia) na Steven Nemes (kushoto)
    Wadau waliohudhuria droo hiyo leo studio za Azam Sports 2 

    RATIBA KAMILI RAUNDI YA PILI AZAM SPORTS FEDERATION CUP
    Ruvu Shooting Vs Madini FC 
    Abajalo Vs Tanzania Prisons
    Njombe Mji Vs Mji Mkuu
    Singida United Vs BodaBoda
    Mwadui FC Vs Pepsi
    Maji Maji FC Vs New Generation
    Boma FC Vs Ndanda FC
    Stand United Vs AFC Arusha
    Burkina Faso FC Vs Lipuli FC
    Green Worriers Vs Simba SC
    Azam FC Vs Area C
    Yanga SC Vs Reha FC
    Mbeya City Vs Ihefu
    Villa Squad Vs Mtibwa Sugar
    Kagera Sugar Vs Makambako
    Makanayagio Vs Mbao FC 
    JKT Mlale Vs KMC
    Ambassador Vs JKT Oljoro
    Mshikamano Vs Polisi Tanzania
    Rhino Vs Alliance 
    Ashanti United Vs Friends Rangers
    Toto Africans Vs Eleven Stars
    Maji Maji Rangers Vs Mbeya Kwanza
    Milambo FC Vs Buseresere FC
    African Lyon Vs Kiluvya United
    Biashara United Vs Mawenzi Market
    Mvuvumwa Vs JKT Ruvu
    Coastal Union Vs Dodoma FC
    Polisi Dar Vs Mgambo JKT
    Kariakoo United Vs Transit Camp
    Shupavu Vs Real Moja Moja
    Mufindi FC Vs Pamba SC 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA NA SIMBA WAPATA VIBONDE KOMBE LA AZAM SPORTS FEDERATION Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top