TIMU ya Paris Saint-Germain imefanikiwa kutwaa Taji la Mabingwa Ufaransa, maarufu kama Champions Trophy baada ya ushindi wa 4-0 dhidi ya Nantes Jumapili Uwanja wa Bloomfield Jijini Tel-Aviv nchini Israel.
Mabao ya PSG yamefungwa na Lionel Messi dakika ya 22, Neymar mawili dakika ya 45 na ushei na lingine dakika ya 82 kwa penalti, wakati la tatu limefungwa Sergio Ramos dakika ya 57.
0 comments:
Post a Comment