• HABARI MPYA

    Saturday, October 18, 2014

    WELBECK AINUSURU ARSENAL KUZAMA KWA HULL CITY EMIRATES

    MSHAMBULIAJI Danny Welbeck ameendelea kuonyesha umuhimu wake kwenye kikosi cha Arsene Wenger baada ya usiku huu kuifungia bao la kusawazisha katika sare ya 2-2 na Hull City.
    Katika mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Emirates, London, Alexis Sanchez alitangulia kuifungia Arsenal dakika ya 13, kabla ya Mohamed Diame kuisawazishia Hull dakika ya 17.
    Abel Hernandez akaifungia Hull bao lililoelekea kuwa la ushindi dakika ya 46 kabla ya Welbeck kuinusuru Arsenal kulala dakika ua 90 na ushei.
    Kikosi cha Arsenal kilikuwa; Szczesny, Bellerin, Mertesacker, Monreal, Gibbs, Flamini/Ramsey dk63, Wilshere/Campbell dk69, Oxlade-Chamberlain, Cazorla, Alexis na Welbeck.
    Hull: Harper/Jakupovic dk43, Chester, Davies, Dawson/Bruce dk84, Elmohamady, Huddlestone, Livermore, Robertson, Ben Arfa na Hernandez/Ramirez dk63.

    Danny Welbeck akiinua mpira kumtungua kipa wa Hull, Eldin Jakupovic kuipatia sare ya 2-2 Arsenal 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WELBECK AINUSURU ARSENAL KUZAMA KWA HULL CITY EMIRATES Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top