• HABARI MPYA

    Tuesday, October 14, 2014

    NEYMAR AFUNGA ZOTE NNE BRAZIL YA DUNGA IKIICHAPA JAPAN 4-0

    MSHAMBULIAJI Neymar amefunga mabao yote manne Brazil ikishinda 4-0 dhidi ya Japan katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliomalizika hivi karibuni mjini Singapore na kumpa raha kocha mpya wa timu hiyo, Carlos Dunga. 
    Neymar anayechezea Barcelona, alifunga mabao hayo katika dakika za 18, 47, 77 na 81 na sasa anafikisha jumla ya mabao 40 aliyoifungia Brazil katika mechi 58.
    Kiungo wa zamani wa Manchester United, Shinji Kagawa na nyota wa Milan, Keisuke Honda walianzia benchi kwenye kikosi cha Japan. 
    Kikosi cha Brazil kilikuwa: Jefferson; Danilo, Miranda, Gil, Filipe Luís; Luiz Gustavo, Elias, Willian, Oscar; Diego Tardelli na Neymar
    Japan: Kawashima, Ota, Sakai, Shiotani, Morishige, Tanaka, Taguchi, Morioka, Shibasaki, Okazaki na Kobayashi. 
    Kaka akimpongeza Neymar baada ya kufunga leo
    Neymar akimtoka mchezaji wa Japan leo
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NEYMAR AFUNGA ZOTE NNE BRAZIL YA DUNGA IKIICHAPA JAPAN 4-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top