BEKI wa Manchester United, Nemanja Vidic ametangaza kuondoka katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu baada ya kukataa kuongeza Mkataba.
Kocha David Moyes alikuwa tayari kumbakiza Nahodha wake huyo Old Trafford, lakini Vidic, anayemaliza Mkataba mwishoni mwa msimu, ameamua kuondoka baada ya kuitumikia Manchester kwa miaka minane.
Mserbia huyo ameshinda mataji 15 tangu awasili klabu hiyo akitokea Spartak Moscow ya Urusi kwa ada ya uhamisho ya Pauni Milioni 7, Januari mwaka 2006, na baadayekuwa Nahodha chini ya kocha Sir Alex Ferguson.
Katika taarifa yake, Vidic amesema: "Ni mwaka wa mwisho wa Mkataba wangu na nimekuwa na miaka minane mizuri hapa.
Anaondoka: Beki wa United, Vidic (kushoto) ametangaza kuondoka mwishoni mwa msimu
Aliposajiliwa: Vidic alisainiwa na kocha wa zamani wa United, Sir Alex Ferguson kutoka Spartak Moscow Januari mwaka 2006
Vidic amaichezea takriban mechi 400 Man United
Tabasamu: Vidic akiinua Kombe la ubingwa wa Ligi Kuu msimu wa 2010-11, taji lililoweka rekodi ya klabu hiyo kutwaa mara nyingi zaidi, mara19
MATAJI ALIYOSHINDA VIDIC MAN UNITED
MATAJI YA TIMU:
Ligi Kuu: 2006/07, 2007/08, 2008/09, 2010/11, 2012/13
Ligi ya Mabingwa Ulaya: 2007/08
Kombe la Ligi: 2005/06, 2008/09, 2009/10
Ngao ya Jamii: 2007, 2008, 2010, 2011, 2013
Klabu Bingwa ya Dunia ya FIFA: 2008
TUZO BINAFSI;
Mchezaji Bora wa Mwaka wa PFA: 2006/07, 2007/08, 2008/09
Mchezaji Bora wa Mwaka wa Ligi Kuu Engand; 2008/09, 2010/11



.png)
0 comments:
Post a Comment