• HABARI MPYA

    Tuesday, February 04, 2014

    LOGARUSIC APATIWA BONGE LA NYUMBA UFUKWENI MWA BAHARI

    Na Saada Akida, Dar es Salaam
    KLABU ya Simba, imefanikiwa kumpatia nyumba ya kuishi, kocha wake Zdravko Logarusic maeneo ya Kunduchi karibu na ufukwe wa bahari ya Hindi, mkabala na hoteli ya Wet n Wild, Dar es Salaam.
    Logarusic aliyesaini mkataba wa kufundisha timu hiyo ya Simba kwa miezi sita tangu ametua hapa nchini akitokea nchini kwao Croatia alifikia hotelini.
    Simba raha; Logarusic atakuwa anaishi ufukweni mwa bahari ya Hindi, eneo la Kunduchi, Dar es Salaam

    Hata hivyo, Loga ataendelea kubaki hotelini hadi pale atakaponunuliwa fenicha za nyumba hiyo yake mpya, atakayokuwa akiisha kwa kipindi chote atachokuwepo hapa Simba SC.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LOGARUSIC APATIWA BONGE LA NYUMBA UFUKWENI MWA BAHARI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top